MASHINDANO ya urembo kumsaka kisura wa Tanga (Miss Tanga 2007) yatakujia kupitia kampuni ya Five Brothers Entertainment ya hapa jijini Tanga. Kampuni hii inachukua jukumu hili zito ikiwa ni mara ya tatu katika historia yake. Lengo letu ni kuonyesha utofauti uliopo kutoka kwetu na wengine na safari hii tunataka kuhakikisha kuwa Tanga inatoa wawakilishi walioandaliwa vema, wanaoweza kutoa changamoto katika mashindano ya dunia. Ni kweli tumedhamiria kushinda taji la taifa na mrembo wetu kufanya maajabu ambayo hayajawahi kufanywa katika Miss World 2007.
Malengo haya ni mazito na hayawezi kukamilika bila ushirikiano wako wewe. Kwanza kabisa binti yeyote mwenye kipaji na mwenye nia ya kufanya maisha katika fani ya urembo. Pili, familia ya binti huyo kwa kutoa sapoti kwa binti yako kushiriki katika kufanikisha azma ya kipaji chake. Tatu, kwako wewe mwanajamii wa Tanga na vitongoji vyake, kushirikiana nasi kuanzia zoezi la kuwapata wawakilishi toka unapoishi na pia kuingia katika kumbi za kuwaandaa na kupata burudani mbalimbali ambazo tutakuandalia kwa ubora wa kutosha.
Kampuni ya Five Brothers Entertainment inahusika na utayarishaji wa matamasha mbalimbali. Tuna uzoefu katika shughuli hizi hapa nchini na hii ni fursa adimu na muhimu kwako mkazi wa Tanga kushiririkiana nasi, kufahamiana nasi na pia kupata kazi za matunda ya kampuni yetu. Huu ni mwanzo mwema wa kujenga ushirikiano wetu kwako na kwako kwetu. Tunaamini kuwa ushirikiano huu utazidi kuanzia hapa ambapo utapata fursa ya kutumia huduma zetu na sisi kuendelea kukuthamini kama mtumiaji huduma mwenye taadhima zote.
Shangamoto ni kwa Wadhamini wa shughuli hizi, wakati bendera ya mrembo wetu ikipepea, nao watapepea pia, tunapenda kuwashukuru wadhamini wetu wote, Vodacom Tanzania, ambao ndio Main sponsor, Redds, CRDB Bank, Tanga Fresh, Tanga-Uwasa, GMC Wasanii Promotors, Mwananchi Communications, Clouds FM na Hotel Kola Prieto kwa mchango wao.
Kupitia Gazeti Tando hili, tutatoa fursa kwako kutoa maoni ya mambo mbalimbali. Inaweza kuwa, kutuomba tuwashauri mabinti unaowafahamu ili washiriki katika shindano hili, inaweza kuwa maoni kwa ajili ya mazoezi yetu na pia tutakupa kila hatua ya shindano hili kupitia blog hii. Kama utakuwa na maswali kwa washiriki au sisi waandaaji utatakiwa kutoa maswali yako pia hapa ukifuatia njia nyingine kama simu, e-mail na barua.
Ninakukaribisha sana, shiriki nasi katika kuipa Tanga ramani yake ya heshima hapa Tanzania na duniani. Ahsante!

No comments:
Post a Comment