Tuesday, May 15, 2007

VISU VYA UHAKIKA




Kila siku zinavyosonga mbele ndivyo mambo yanazidi kuongezeka, hapa tunazungumzia mchakato mzima wa kumpata mrembo mwenye viwango kutoka jijini Tanga.
Habari zilizopo ni kwamba baada ya kitongoji cha miss Chumbageni kwenda vizuri, mazoezi ya Vimwana watakaoshiriki shindano la kumsaka Kisura wa Vyuo jijini Tanga (Miss Collage City Centre)yanaendelea katika ukumbi wa Splended wa Jijini hapa na kua kivutio kutokana na mvuto wa warembo shiriki.

Mratibu wa mashindano hayo ya Miss Collage, Maximilian Luhanga anasema kuwa mvuto wa michuano hiyo umetokana na ubunifu wa mwalimu wao pamoja na mipango thabiti ya waandaaji wakishirikiana na kamati nzima ya Miss Tanga.

Miss Collage atapatikana May 18 katika ukumbi wa Habours Club Jijini, Tayari kwa kuingia katika orodha ya watakao wania taji kubwa la mkoa, Miss Tanga 2007 lililopangwa kufanyika June 8 mwaka huu.


MISS TANGA 2007


Mchuano wa Miss Tanga 2007 Umedhaminiwa na Vodacom, Redds, CRDB, Tanga Fresh, Tanga Uwasa, Screen Masterz, Hotel Kola Prieto, Dollywood, GMC wasanii Promotors, Kampuni ya Mwananchi Communication na Radio Clouds Fm.

No comments: