Thursday, April 17, 2008

FAIDIKA



Tukiwa tunasubiri kuanza kwa mchakato mzima wa miss tanga 2007 faidika na promoshen za vodacom ambao ndio wadhamini wa kuu wa mashindano haya. kazi kwako

Wednesday, June 6, 2007

TANGA TUNAWEZA


HUYU bibie anatajwa kuwa ndiye mrembo pekee kutoka mjini Tanga aliyefanikiwa angalau kufika tatu bora katika ngazi ya Kitaifa kwenye mashindano ya Miss Tanzania. Mabibi na mabwana ...huyu ni Mona Koja, Miss Tanzania namba 3, wa mwaka 1996 hapo akiwa na mwanae Ryan. Ingawa Rekodi hiyo ya aina yake mpaka sasa bado haijavunjwa na washiriki yeyote kutoka mjini hapa, imani kubwa ipo kuwa Tanga Tunaweza.

Ingawa Mona hakuvikwa taji la Miss Tanzania, lakini alileta upinzani mkubwa katika mashindano hayo mwaka huo na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu ikiwa ni mara ya kwanza mrembo kutoka Tanga kushika nafasi hiyo, tangu mwaka 1994 ambapo shindano hilo lilipanua utafutwaji wa warembo katika ngazi za Mikoa.

Mrembo huyo ambaye amehamishia makazi yake Uingereza alirudi nchini Desemba 24 mwaka jana na kufanya mazungumzo na Kampuni ya 5Brotherz, alichochangia tunaimani kitasaidia kwenye mchakato mzima wa mishe mishe zetu.

ZAWADI YA MISS TANGA


Kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano ya urembo mkoani Tanga, Mshindi atajinyakulia zawadi ya gari.
Fagilia basi .....

TATU BORA YA MISS VYUO


Hawa ndio walioshika mataji ya miss vyuo, kitongoji kimoja wapo cha miss Tanga 2007
Kati kati anaitwa Victoria Martin ndiye mshindi wa miss vyuo, wa pili kushoto anaitwa Time salum watatu ni Hele Cisary

TANGAZO


Kwa hisani kubwa ya Magazeti ya mwananchi, Tangazo hili limechapishwa humo kwa takriban wiki 6

MCHUANO UKO HIVI


Unadhani nani ataondoka na taji la miss tanga 2007 kati ya hawa?