Friday, April 18, 2008
Thursday, April 17, 2008
FAIDIKA
Wednesday, June 6, 2007
TANGA TUNAWEZA

HUYU bibie anatajwa kuwa ndiye mrembo pekee kutoka mjini Tanga aliyefanikiwa angalau kufika tatu bora katika ngazi ya Kitaifa kwenye mashindano ya Miss Tanzania. Mabibi na mabwana ...huyu ni Mona Koja, Miss Tanzania namba 3, wa mwaka 1996 hapo akiwa na mwanae Ryan. Ingawa Rekodi hiyo ya aina yake mpaka sasa bado haijavunjwa na washiriki yeyote kutoka mjini hapa, imani kubwa ipo kuwa Tanga Tunaweza.
Ingawa Mona hakuvikwa taji la Miss Tanzania, lakini alileta upinzani mkubwa katika mashindano hayo mwaka huo na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu ikiwa ni mara ya kwanza mrembo kutoka Tanga kushika nafasi hiyo, tangu mwaka 1994 ambapo shindano hilo lilipanua utafutwaji wa warembo katika ngazi za Mikoa.
Mrembo huyo ambaye amehamishia makazi yake Uingereza alirudi nchini Desemba 24 mwaka jana na kufanya mazungumzo na Kampuni ya 5Brotherz, alichochangia tunaimani kitasaidia kwenye mchakato mzima wa mishe mishe zetu.
ZAWADI YA MISS TANGA
TATU BORA YA MISS VYUO
Subscribe to:
Comments (Atom)





